Sehemu
ya Pili
Na Aloyce Kalunde
Ukhali gani msomaji wa makala hii, nishukuru kwanza
kwa wote mliotuma maoni yenu kwa email na simu. Maoni yenu nishayafanyia na
ninaendelea kuyafanyia kazi. Ungana name
sasa hasa kwa kuchambua:
KANUNI ZA MSINGI KATIKA NDOA
Mungu ndiye mwanzilishi wa ndoa ambaye
alifunga ya Adamu na Hawa katika bustani ya Edeni (Mwa.2:18-24). Tukitaka kuelewa muungano huu wa mume na mke ni
muhimu tuelewe kanuni za msingi za kibiblia. Kuna maneno matatu ambayo ni
muhimu tuangalie kwa kifupi maelezo yake.
1. Kuondoka (leaving).
Hii humaanisha kuwa wanandoa yaani mme
na mke, wote wawili huhitaji kuamua nyumba na familia yao ni kwao wawili tu,
hata kama wanahitajika kuwaheshimu wazazi na jamaa wote wa pande zote mbili. Tangu
siku ya kufunga ndoa wote wawili wafahamu kuwa mahali pa kwanza pa kupata
msaada na ushauri ni kutoka kwa mwenzi wake. Mume na mke wanakuwa na umoja
mkamilifu. Wajibu wao wa kwanza unakuwa kwao wenyewe. Wanapooana kipaumbele ni
kwa mke au mume wa kwanza.
2. Kuambatana (cleaving).
Neno hili linatokana na neno la
Kiebrania ‘dabag’ lenye maana ya
kushikamana na mwenziwako wa ndoa na kuwa kitu kimoja. Neno hili ni zito sana
katika maana yake ya asili, yaani Kiebrania. Humaanisha kugandamana, kushikamanan au kung’ang’aniana kama stempu
inavyogandamana na barua. Ukijaribu kutenganisha stempu na barua vyote
huchanika na kuharibika. Kimatendo inamaanisha kuwa na uamuzi wa kumchagua
mwenzi wako kuwa rafiki na mpenzi wako na anakuwa wa kwanza wa kushauriana
naye.
Kuambatana ni kujitoa kabisa kwa
mwenzio. Hili lina maana ya ahadi, uhakikisho kwa mwenzio. Kwa hiyo kuambatana
ni uamuzi wa dhati na wa kukusudia ili kutengeneza muungano. Ndoa yenye afya ni
ile ambayo ina muungano sahihi uliotokea kati ya mwanamke na mwanaume.
3. Kuwa mwili mmoja (one
flesh).
Kuwa mwili mmoja maana yake ni kuwa na
upendo wa ndani na kuunganika katika hisia, utu, na ushirika mtakatifu wa tendo
la ndoa (1Kor.6:16; 7:2-5). Hili linahusu hasatendo la ndoa. Kujamiiana kwa
wanandoa ni kitu kitakatifu na mapenzi ya Mungu.
Yapo mambo mengi ya muhimu watu
wanapokuwa mwili mmoja: Kuleta umoja wa nafsi na roho. Tendo la ndoa katika
mwanadamu hugusa kila sehemu ya utu wake. Kufanyika mwili mmoja haihusishi tu
hali ya mwili, bali hisia na roho kwa kifunganisho cha ukaribu wa faragha. Pia
tendo hilo huongeza furaha kwa wapenzi hao wawili.
ZIJUE TOFAUTI KATI YA MUME NA MKE (GENDER
DIFFERENCES)
Kuna ukweli kwamba mwanaume na mwanamke
wanaweza wasijuane hali zao za tofauti kijinsia katika maisha yao na ikabaki
kuwa ni siri. Inawezekana ni namna ambayo Mungu ameifanya, vinginevyo maisha
yangekuwa ni kitu cha kuchosha sana kwa mwanadamu bila kuwa na kazi ya kutaka
kugundua mambo mapya.
A. Tofauti katika mawasiliano
1. Wanawake:
Þ
Wanawake
wana uwezo mkubwa wa kuhisi mambo au hali halisi ya jambo fulani (jema au baya)
kuliko wanaume. Ndiyo maana inaaminika kuwa wanawake wanamilango sita ya
fahamu.
Þ
Katika
mazungumzo wanawake hupenda kuzungumzia mambo yanayo gusa hisia, mahitaji, matumaini,
ndoto, mambo yanayoleta hamu (wants),
shida mabalimbali, suluhisho katika shida na mambo yoyote yanayo husu
mahusiano. Wanawake hutaka wanaume wawasikilize na kuwajibu. Hupenda waume zao
wawaone ndani ya mioyo yao na fahamu zao (minds)
na kisha kujua kile kinachowafanya wafurahi au wawe na huzuni. Wanawake humtaka
mwanaume ambaye atajitoa kwake siku zote za maisha yake, anayetunza uaminifu
kama jiwe kuu la pembeni la uhusiano. Wanapenda mwanaume anayefurahia maisha
pamoja nao, anayejua kucheza, aliyetayari kujiona kuwa anao upungufu
mahalifulani. Wanamtaka mtu aliye mbunifu, asiye mwoga, mwenye akili na
mwajibikaji katika maisha yake.
Þ
Mwanawake
anamtaka mume aneyeweza kujalimahitaji yake kwa undani sana, atakaye tambua
mahitaji yake, aliye wazi katika msimamo wake.
Þ
Wanawake
kwaasili ni watu wa kupenda na ni wasiri. Waandishi mbalimbali, washairi na
wanasaikolojia waliojaribu kulijibu swali gumu katika kutafakari juu ya
wanawake huhitaji nini hasa, bila mafanikio.
Þ
Mwanamke
ni kiumbe wa ajabu (complex and intricate
being). Mwanamke anahitaji shukrani toka kwa mumewe anapofanya jambo jema.
Wanawake ni watu wa hisia za ndani sana, huguswa na kila jambo linalofanyika.
Þ
Wanawake
hujihusisha zaidi na kutengeneza mahusiano ya karibu ambayo yanashikiliwa
pamoja na hali ya kiunganishi. Hii inamaana wanawake wanafurahia katika hali ya
kuunganika na kuambatana katika mahusiano. Kwa maana nyingine wanawake
hufurahia kuwa na mahusiano ya ndani. Hii ndiyo sababu umuhimu wa kuolewa kwa
wanawake ni suala la kipaumbele kwa sababu utambulisho wa mwanamke unapatikana
katika muunaganiko wa mahusiano. Wanawake huolewa kwa lengo la usalama na
kupata watoto.
Þ
Wanajisikia
vizuri kuwa wanawake.
2. Wanaume
Þ
Wanaume
hupenda wanawake wenye kuwahudumia na kuwafariji, wenye kujishusha, wasiojikweza
au kuhukumu, wenye ujuzi wa maisha.
Þ
Hupendelea
mwanawake anayevutia. Kwa kawaida mwanaume husisimuliwa kimapenzi kwa
kumwangalia mwanamke kwa macho. Hivyo hupenda mke wake awe katika mwonekano
mzuri na wa kuvutia.
Þ
Hitaji
la msingi la mwanaume ni kutoshelezwa katika tendo la ndoa. Inasemekana
kitaalam kuwa mwanaume akikaa muda mrefu bila kufanya tendo la ndoa toka kwa
mke wake mambo yafuatayo yanaweza kutokea:
Ø
Mume
kushindwa kuongea kwa uchangamfu kama alivyo zoea.
Ø
Mume
kuumwa kichwa na kupata homa.
Ø
Mume
kuwa mkali nyumbani na nje.
Ø
Hukosa
hamu ya kula.
Ø
Anaweza
kuwa na ugonjwa wa tumbo kushika, kukosa haja kubwa.
Ø
Kuwa
na ugonjwa wa mapigo ya moyo, kushuka au kupanda kwa sababu ya mawazo mengi
ambayo hawezi kuyaeleza wazi wazi.
Ø
Anaweza
kumsingizia mke wake na kumpa majina ya ajabu na kumdhalilisha mbele za watu.
Ø
Mume
anaacha kutoa mahitaji ya nyumbani mwake kwa kutaka kumkomoa mke wake.
Ø
Mwili
wa mwanaume hutengeneza mbegu za kiume ambazo zimechanganyikana na madini ya
chokaa (calcium). Chokaa inapolundikana
bila kupata njia sahihi ya kutoka yaani ya tendo la ndoa, husababisha mrija wa
haja ndogo (urethra) kubanwa hata
kuziba. Matokeo mwanaume hupata ugonjwa wa mshipa au ugonjwa wa wazee.
Ø
Mume
bila mwili wa mke wake kwa muda mrefu akili zake si timamu, akili zake
hazitafanya kazi vizuri.
Ø
Sukari
mwilini kupanda na kushuka.
Þ
Wanaume
si watu wa mahusiano kama wanawake.
Þ
Wanaume
ni watu wanaoshughulika na vitu, shughuli nyingi na mipango mingi ya kazi. Si
watu wa kuonyeha hisia zao kwa wepesi.
Þ
Wanaume
hujiona kukomaa wakati wanaweza kujitenganisha wenyewe kama watu binafsi. Huwa
wanathamini kuwa huru na kuwa na utawala kama njia ya kujisikia kukamilika na
kuweza kutembea kwa ujasiri katika maisha.
B. Tofauti katika mahitaji makuu
Yako mahitaji
mengi sana ya muhimu kwa wanandoa, lakini katika hayo yapo yaliyo ya msingi
zaidi ambayo hutofautiana kati ya mwanaume na mwanamke katika vipaumbele.
1. Wanaume
Kutoshelezwa
katika tendo la ndoa.
Rafiki wa
kustarehe naye.
Mwenzi au mke
anayevutia.
Msaada wa mambo
ya nyumbani.
Kuheshimiwa na
kuthaminiwa.
2. Wanawake
·
Kupendwa
kwa upole.
·
Maongezi
ya kirafiki.
·
Uaminifu
na uwazi.
·
Msaada
wa kifedha.
·
Kujitoa
katika familia.
KANUNI ZA NDOA NA NYUMBA
Kwa kuwa ndoa ni mahusiano kati ya mume
na mke ni muhimu kutunza ili izidi kudumu. Zifuatazo ni amri kumi kwa kila
mwanachama.
A. Amri Kumi za Mwanamke.
1.
Mpende
Bwana Mungu kwa moyo wako wote, kwa akili zako zote, nafsi yako yote na
kumpenda mume wako kwa nguvu zako zote ila isiwe kama umpendavyo Mungu wako
(Kumb.6:5).
2.
Kwa
furaha mtii mume wako kama kumtii Kristo (Efe. 5:22).
3.
Fanya
bidii kuutawala ulimi wako, kuwa mwangalifu mbariki nakumtia moyo mume wako.
(Mith. 31:26).
4.
Fanya
bidii kujitunza na nyumba yako ipendeze na kuvutia (Mith.31:27, 28).
5.
Tunza
furaha ya moyoni katika ratiba ya siku nzima kwa kazi ulizo nazo (Kol. 3:17).
1.
Usiruhusu
wivu na uchoyo kuwa asili yako (Mith.6:34).
2.
Mpende
mume wako wala usimlinganishe na wengine, kwa uaminifu mwitikie na kumheshimu
(Efe.5:33).
3.
Mtukuze
Mungu kule kuitwa mwanamke na uzuri wa thamani hiyo kuliko maisha yenyewe
(Mith.12:4).
4.
Pandikiza
kwa watoto wako upendo, heshima na adabu kwa baba yao (Mith. 22:6).
5.
Usihofu
makosa na kukosea (Mith. 24:24; 27:15).
B. Amri Kumi za Mwanaume
1.
Mpende
mkeo kama Kristo alivyolipenda kanisa, uwe tayari kuutoa uhai wako kwa ajili
yake ili aweze kukua katika Kristo (Efe. 5:25).
2.
Mfikirie
na kumtia moyo kwa kuwa Mungu hakumkusudia wajibu mzito (1Pet. 3:7).
3.
Kamwe
usiwe na uchungu moyoni kwa maakosa ya mke, bali msamehe kama Kristo
alivyokusamehe wewe (Efe. 4:32).
4.
Mwongoze
mke wako na familia katika njia za haki, waambukize maisha ya kiroho na hofu
kwa Mungu (Efe.5:22).
5.
Uwe
kichwa cha familia, ili uwapatie ulinzi unaotakiwa, upendo na ulinzi wa kibaba
kama Mungu alivyokusudia (1Kor. 11:3).
6.
Ishi
kwa furaha na mke wako ukijua huyo ni zawadi kwako kutoka kwa Mungu (Mwa.
2:18).
7.
Mbariki,
mtukuze na kumsifu mke wako, kwamba hakuna kama yeye duniani (Mith. 31:28, 29).
8.
Mwamini
mkeo ili kwamba yeye awe mke ambaye Mungu anataka uwe naye (Mith. 31:11).
9.
Kwa
upendo mwambie mke wako matakwa yote kwa kufanya kwa matendo, hivyo onyesha
shukrani zako kwake (Efe. 4:29).
10.
Jitunze
mwenyewe kwa ajili ya mkeo, jitolee mwenyewe kwake tu (Rum.12:10).
Toa
maoni yako kupitia
Email:Kalunde47@gmail.com
+255 783 700083
+255 653 700083
Comments
Post a Comment