VITENDO VYA UTESAJI, UNYANYASAJI VYASHITUA BUSEGA
AFUNGWA KAMBA MIGUU, MIKONO NA SHINGONI
Na Shushu
Joel, Busega
WANANCHI wilayani
Busega mkoani Simiyu katika kata
ya kabita kijiji cha nyakaboja wamekasilishwa na ukatili na unyanyasaji
uliofanywa na Nyafulu (Neema) Makoba
ambaye ni mama mzazi wa Sikolastica Paul mkazi wa kijiji cha nyakaboja wilayani busega.
Mariam Joans
ni jirani wa mama huyo anaeleza kuwa ni kawaida yake Neema Makoba kumtesa mototo
huyo kwani mara nyingi tumekuwa tukisikia sauti ya motto huyo akiwa analia toka
ndani, Mimi na mmewangu tulijaribu kumkanya lakini alishindwa kabisa kutuelewa
Jana majira
ya saa 1 asubui nilisikia kelele ya motto Scolastika akilia kwa sauti ya juu
sana na ndipo nilimwamuru mume wangu twende tukamsaidie mtoto huyo mara baada
ya kufungua mlango tulimkuta amefungwa na kamba miguuni,mikononi na shingoni na
kasha kamba hiyo kufungwa kwenye nondo za dirishani.
Kutokana na hali hiyo kuiona mme wangu alimkimbilia mtendaji wa kijiji Mariam Kagusa naye alipofika alimuona motto huyo akiwa katika hali hiyo huku mda huo mama mzazi wa binti huyo hakuwepo nyumbani kwake. Mtendaji wa kijiji aliwaamuru wananchi kuweza kumchukua mtoto na kumpeleka kwa Afisa ustawi wa jamii wa Busega Grace Mmasi naye kuamuru mama huyo aweze kupelekwa katika kituo cha polisi.
Afisa ustawi huyo alisema kuwa ni kitendo cha kinyama kwa mama huyo kuweza kumfanyia mtoto huyo asiyejua kitu chochote masikini. Mara baada ya kuhojiwa na mwandishi wa NIPASHE mama huyo alisema kuwa alimpatia adhabu hiyo scolastika kutokana na kupotea kwa kiasi cha shilingi elfu tano ndani.
Kwa upande
wake binti Scolastica Paul anasema kuwa si kweli yeye hakuchukua pesa hiyo kwani
mama ni muongo na ni mda mrefu amekuwa akinitesa na kuninyima chakula na hata
kunifungia kwa nje na yeye kuweza kwenda kuangalia video katika mabanda.
Aliongeza
kuwa ndani mwao kulikuwa na kiaasi cha shilingi mia mbili mbili yaani 400 sasa
sijui ni kwa nini mama anashindwa kusema ukweli juu ya hili, kwani hata shule
kashindwa kunipeleka wakati babu alimpatia pesa ya mahitaji yote.
Alipofika
Babu na mjomba wa mtoto huyo walimchukua na kuondoka naye huku baba mzazi wa
neema akisema kuwa anaiomba mahakama kuweza kutoa fundisho kwa bintiyake kwani
ni muuaji na pia aliweza kumchukua mjukuu wake na kuahidi kumpeleka shule.
Polisi
wilayani Busega inakamilisha hatua za kisheria ili iweze kumfikisha mahakamani.
Comments
Post a Comment