TUNZA NDOA YAKO

Sehemu ya Kwanza

Na Aloyce Kalunde

Neno ndoa linatafsiri mbalimbali kulingana na mila ya mahali fulani. Lakini kwa ujumla ni muungano halali wa kijamii, kisheria wa watu wawili wa jinsia tofauti, mume na mke walio amua kuishi pamoja kwa hiari yao ili kutimiza kusudi la Mungu. Huu ni uhusiano wa ndani sana unaohusisha urafiki na tendo la ndoa.

KWA NINI KUOA/KUOLEWA?
Katika mazingira tofauti tofauti watu huoa au huolewa kwa sababu mbalimbali kama za kijamii, kisheria, kupendana, kujamiiana, kihisia, kiuchumi, kiroho na kidini. Lakini jambo moja kuu ni kuwaleta pamoja watu wawili waliotofauti ili hatimaye waweze kushirikiana kwa pamoja mali zao na pia uwezo na vipaji vyao katika maisha. Wanaingia katika hali ya kushirikiana hali zote za maisha, njema au mbaya, furaha na huzuni, hofu, mafanikio nk.

Mahali pengi duniani na hasa Afrika, kupata watoto katika ndoa huwa ni jambo linalochukua umuhimu mkubwa katika ndoa. Katika mazingira kama haya ndoa haiitwi imekamilika bila kuwa na watoto. Hutokea mahali pengine wanaume kuoa mke mwingine endapo mke wa kwanza hana uwezo wa kuzaa mtoto. Ikumbukwe kwamba katika Biblia ndoa zilikuwepo zenye watoto na zisizo na watoto. Hivyo dhana hiyo siyo sahihi kwamba ndoa bila watoto siyo ndoa, Biblia haisemi kitu cha namna hiyo.

Muungano huu wa watu wawili hukamilishwa kwa tendo la ndoa ikiwa ni njia ya kuimarisha uhusiano wao kwa namna ya kipekee sana kiasi kwamba hujisikia kuwa mwili mmoja.

Mungu alipomuumba Eva (Hawa)  na kummpa Adamu alitaka wawe na ushirika na kila mmoja kumtambua mwenziwe na kutegemeana na kumtegemea Mungu. Ushirika wao huu ungekamilishwa kwa tendo la ndoa. Tutaangalia kwa undani habari hizi katika somo husika. Sababu zingine za watu kuoa au kuolewa ni:

Ni tiba ya upweke
Watu huoa na kuolewa ili kuondoa upweke. Adamu alipokuwa peke yake alikuwa na huzuni na upweke. Lakini alipokuja Hawa upweke uliondoka kwa vile alimpata mwenzi wake ambaye hakupatikana miongoni mwa wannyama ambao aliishia kuwapa majina tu na siyo kupata ushirika wowote (Mw.2:18).

Huleta furaha na raha
Watu huamua kuishi pamoja ili kupata furaha na raha. Mfalme Abimeleki alitambua kuwa Isaka na Rebeka walikuwa ni mtu na mkewe alipowaona wakicheza chumbani wakifurahiana.

Kutuepusha na tamaa na uzinzi
Paulo anasema kila mtu na awe na mke wake mwenyewe ili aweze kupata raha ya tendo la ndoa kwa mke wake wa ndoa na si vinginevyo. (1Kor.7:2).

Ili kukamilishwa na mwenzi wake wa ndoa
Mwanaume ana pengo ambalo linatakiwa kujazwa na mkewe na kwa mwanamke vivyo hivyo. Kilammoja hajakamilika bila mwenzi wake wa maisha (Mwa. 2:21-22); Mat. 19:3-6). “Adamu peke yake alikuwa hajakamilika , alikosa mwenzi wa kumfanania mpaka alipoumbwa Hawa.”

Ndoa huleta heshima katika jamii
Watu wanaoana ili kupata heshima katika jamii, kwani mtu aliyeoa au kuolewa ana heshima ya tofauti na yule ambaye hajaoa au kuolewa.

Ndoa huleta usalama na ulinzi kwa wanandoa
 Kuoa na kuolewa katika jamii ni ulinzi. Kuna kuogopwa kwa wanandoa katika jamii husika (Yer.31:22; 1Kor.7:37).

Ili kuendeleza uumbaji wa Mungu kwa kuzaliana
Mungu anapenda tuwe na familia na watoto ambao ni baraka kutoka kwa Mungu (Mwa.1:28).

MAMBO YANAYOHARIBU NDOA

Kuna mambo yanayoweza kuharibu ndoa yako kama hutakuwa makini. Kuna sababu kadha wa kadha zinazochangia kuvunjika kwa ndoa:

Kukosauaminifu katika ndoa.
Baadhi ya wanawake na wanaume (wanandoa) huanza kuwa na wanaume au wanawake wa pembeni, hili ni kosa kubwa katika mpango wa ndoa aliouanzisha Mungu.

Kutokumpenda mwenzi wako wa ndoa.
Kuwapenda watu wengine kuliko mwenzi wako wa ndoa hupelekea kuvunjika kwa ndoa. Ikitokea mume anawapenda rafiki zake au jamaa yake kuliko mkewe, na vivyo hivyo mwanamke, ndoa hiyo huwa iko hatarini kuvunjika.

Kukosekana kwa mawasiliano mazuri.
Hali hii huleta kutokuelewana kwa wanandoa, yaani kila mmoja kuwa mbinafsi na kujali matakwa yake tu. Mawsiliano huweza kuharibiwa na:
Ø Matakwa binafsi.
Ø Kutokuwa wazi baiana ya wanandoa.
Ø Kupuuzia mambo.
Ø Kutopeana nafasi ya kusema na kusikilizana baina ya wanandoa.
Ø Kuskiliza zaidi kitu cha nje na kuamini kuliko anachokuambia mwenzio.

Kutokuwa na mipaka katika ndoa.
Watumishi wanyumbani, mawifi, mama mkwe wa pande zote ni lazima wawekewe mipaka katika ndoa. Kwa kuwa ndoa ni ya watu wawili, mtu wa tatu ni ibilisi.

Kutokuwa na umoja.
Kukosekana kwa umoja au ushirika kwa wanandoa hufungua mlango wa ndoa kuvunjika. Hii ni pamoja na kuwa na ubinafsi na kulimbikiza vitu moyoni kwa kukosa roho ya msamaha baina yao.

Kuyumba kwa uchumi.
Uchumi unapoyumba huweza kutokea kutokuelewana kwa wanandoa kwa sababu ya kukosekana kwa mahitaji mbalimbali nyumbani.

Ugumba au utasa.
Hali hizi huondoa amani katika ndoa na kusababisha hata kuvunjika kwa ndoa nyingi.

Shida za mateso.
Ugomvi, shida, manyanyaso, vitu hivi vikiwepo mara kwa mara huweza kupelekea ndoa kuvunjika.

Kutokuomba.
Kutoombea ndoa huweza kumpa Ibilisi nafasi ya kuivuruga na kuivunja (Sam. 12:23).

Kunyimana unyumba.
Kumnyima mwenzi wako wa halali tendo la ndoa kunaweza kutoa mwanya kwa mwenzi wako kumtafuta mwingine atakayemridhisha na kumfurahisha katika tendo hilo. Hasara za kunyimana tendo la ndoa:
Ø Ugomvi mkubwa hutokea baina ya wanandoa.
Ø Kutoka nje ya ndoa.
Ø Kutopendana na kuchukiana.
Ø Kutoheshimiana.
Ø Kiburi na kutoelewana.
Ø Kuvunjika kabisa kwa ndoa

Kutoaminiana.
Hapa ni chanzo cha kuharibu ndoa, kwamaana imani inakosekana pande zote mbili.

Kukaa muda mrefu mbalina kumwacha mwenzi wako wa ndoa.
Hali hii huweza kufungua mlango wa uzinzi kwa wanandoa wengi na hivyo kusababisha kuvunjika kwa ndoa.

Kukosa uvumilivu.
Kushindwa kuvumiliana katika mambo mbalimbali yanajitokeza katika ndoa kwa mwenzi wako. Hii ni sababu moja wapo ya kuvunjika kwandoa.

Kukosa muda wa kukaa pamoja na familia yako.
Kutopeana nafasina mwenzi wako ya kuongea na familia hujisikia kama hathaminiwi, na hivyo kuvuruga ndoa.

Tuma maoni yako kwa:
+255 783700083
+255 653 700083



Comments