Na Shushu
Joel, Busega.
0782 466366
Kikundi cha
watu wanaoishi na maambukizi ya ugongwa wa ukimwi toka katika wilaya ya busega
mkoa wa simiyu wametoa ombi lao kwa serikali ya Tanania kwa niaba ya wenzao
wote walio na ugonjwa huo na tayari wamejiunga katika matumizi ya ARV.
wathibiti wa maambukizo ya ukimwi wilayani busega pia ni waathirika wa ugonjwa huo.
Kikundi
hicho chenye jin la kamati ya kuthibiti maambukizi ya ukimwi wilayani busega
(SIMAKI) chenye wanachama wasiopungua 50 kimetoa lalamiko kwa serikali kwa
kutokupatikana kwa dawa za kupunguza makali kwa waathiria katka siku ya ukimwi nchini.
Wakizungumza
kwa wakati tofauti tofauti walisema kuwa kwa sasa kumekuwa na uhaba mkubwa sana
katika kupewa kwa dawa hizi ukilinganisha na miaka ya nyuma mgonjwa alikuwa
anapewa dawa za kumeza za mwezi mzima lakini kwa sasa hivi imekuwa sivyo kwani
tunapewa dawa za kumaliza wiki moja hivyo hali hii sisi inatuumiza sana
ukilinganisha na pato letu.
Bwana Nandi
Bulengera yeye ni mjumbe katika kamati hii anasema kuwa wanakumbana na
changamoto nyingi sana katika jamii inaowazuguka ikiwemo ya kubaguliwa,
kutothaminiwa lakini yeye anaona hali hii ni ya kawaida kwake na anahitaka
serikali kuweza kuwawezesha wagonjwa hata wa kuwapa matunda kwa kila mwisho wa
mwezi ili afya zao ziweze kuwa fiti zaidi.
Bi Penina Palapala
yeye alianza kutumia ARV mwaka 2006 mpaka sasa anaendelea vizuri sema
analalamikia kwa watu kuona aibu kupima afya zao ili waweze kujitambua kama
wanamaambukizi au vp, Hivyo B I penina ameitaka serikali kuendelea kutoa nafasi
na kipaumbele kwa watu walio na maambukizi ya ukimwi hapa nchini kwa kuwapa
dawa za kutosha na hata kutoa vyakula kwa wale wasiojiweza kwani dawa hizi
zinanguvu sana hivyo inahitaji kupata lishe bora.
Pia
mwanachama mwingine ni Sospiter Majige anaeleza kuwa alianza kutumia dawa za
ARV mwaka 2007, Hivyo aliitaka serikali kuweza kuongeza juhudi za kuongeza
uwepo wa vituo vingi vya utoaji huduma kwa watu wenye maambukizi ya ukimwi.
Wajumbe wanaoamasisha watu kupima ukimwi kwa hiari wilayani Busega na
wao pia ni waathirika wa ugonjwa huo.
Upande wa
serikali iliwakilishwa na makamu mwenyekiti wa halmashaul ya busega Bw, Mngumbi
Mojo anasema kuwa anaishukuru sana kamati ya kuthibiti maambukizi ya ukimwi
wilayani busega kwa utendaji mzuri wa kazi zao kwa kuhamasisha watu kupima na
kutambua afya zao .
Mojo
aliongeza kuwa tatizo bado lipo kwa wakazi wanaoishi kando kando mwa ziwa
(mwaloni) hawa ndiyo chanzo cha maambukizi ya maradhi katika wilaya yetu hivyo
basi aliitaka serikali kuweza kuongeza juhudi binafsi ili kuweza kupambana
nawatu hawa.
Tanzania
mpya bila maambukizi ya ukimwi inawezekana ndiyo kauli ya makamu mwenyekiti
huyo.
Comments
Post a Comment