NSSF YAJITOSA KUTATUA KERO ZA WAVUVI NCHINI.



Na Shushu joel
Busega, Simiyu




Shirika la mfuko wa hifadhi ya jamii nchini (NSSF) wameamua kujitosa ili kuweza kupambana na kero zot za wavuvi nchini bila kubagua wala upendeleo wowote ule .
Hya yamesemwa leo katika kijiji cha Ihale kata ya kiloleli wilayani Busega mkoani simiyu na Meneja wa Nssf mkoa wa shinyanga na simiyu Bw, James Mashinga  wakati akitoa semina kwa wavuvi  wa eneo hilo.

Mashinga aliwata wakazi hao wa Ihale waweze kutumia fursa hii ya pekee ambayo imeamuliwa kutolewa na shirika hilo pekee nah ii imetokana na shirika hilo kuona wavuvi,Wakulima na Wafugaji kusahaulika na serikali.

Alisema kuwa watakao jiunga na shirika hili watapata huduma nyingi bure ikiwemo matibabu ya hospital kwa familia yaani Baba, Mama na watoto wasiopungua wanane pia kutokuwepo na fursa za kupewa mikopo ya kipekee kwa wanachama ili waweze kuondokana na masuala ya kuajiliwa na waweze kujiajiri wao wenyewe.

Aidha Mashinga aliwasihii sana wana Ihale kuweza kutumia nafasi hii ya kipekee kwao, hivyo aliwaambia mara baada ya kumalizana na wavuvi watahamia katika sekta nyingine na lengo likiwa ni kuwakwamua katika janga la umasikini.
Kwa upande wake Afisa uvuvi wa wilaya hiyo ya busega Bi Judith Mgaya ameweza kutoa wito kwa wavuvi kuweza kujitokeza kwa wingi ili waweze kupata huduma ya hifadhi ya mfuko wa jamii kwani ni fursa ya pekee kwao kuweza kujikwamua katika hali ya uchumi hapa nchi pia Bi mgaya aliweza kutoa pongezi kwa shirika la Nssf kwa kutambua shida za wavuvi nchini na kuweza kupambana nazo.

Upande wa wananchi wa Ihali waliojitokeza kwa wingi kuweza kujiunga na huduma hizo za kijamii wakisemewa na Bw, Dionis Kabati anasema kuwa wao kama wavuvi wanaishukuru Nssf kwa kuweza kutambua kero zao na hata kupata elimu ya kuwa kuna mambo kama hayo ambayo sisi tulikuwa atuyajui kabisa, Hivyo aliwata viongozi hao wa Nssf kuwa nao karibu zaidi ili waweze kubadilisha maisha yao.

Mwenyekiti wa BMU katika mwalo wa Ihale Bw, Pius mazima anasema kuwa sasa ni wakati mwafaka wa wavuvi kujikwamua na kwa hili hata uvuvi harama utakuwa kikomo nchini.

Comments

  1. Inafurahisha kutupata habari za mkoa wa Simiyu na wilaya zake. Tunaomba ututambulishe wahusika tupate kuwajua.

    ReplyDelete

Post a Comment