TALGWU KUGOMEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA
MITAA,VITONGOJI NA ULE MKUU WA MWAKA 2015.
Na Shushu
Joel
Busega,
Simiyu
Mpango
kabambe unaoandaliwa na Chama cha wafanyakazi wa serikali za mitaa hapa nchini
kimeandaa mipango kabambe ya kugomea kutokushiriki kusimamia wala kupiga kura katika
uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajia kufanyika hapa nchini tarehe
14?12/2014 na uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.
Akifafanua
sababu za kugomea uchaguzi huo kaimu katibu mkuu wa Talgwu hapa nchini Bw,njaa
Kibwana ni kuitaka serikali ya jamhuri
ya muungano wa Tanzania kuweza kukilipa chama chao deni lao la kiasi cha
shilingi billion 18.
Akizungumza
na wanachama wa TALGWU wilayani busega Kibwana aliwataka wanachama hao kuwa na
umoja ili waweze kufanikisha kulipwa kwa deni lao toka serikali npia nao kuweza
kuthaminiwa kama vyama vingine vinavyopata thamani hapa nchini.
Aidha
Kibwana alisisitiza kuwa wanachama sasa inatubidi kuwa wajasiri katika kudai
masilahi yetu sisi wanachama na mwaka huu itabidi tuonyeshe mfano wa kuwa nasi
tunaumuhimu katika serikali sasa tunaelekea kugomea chaguzi zote mpaka tulipwe
madeni yetu alisema naibu katibu mkuu wa huyo hapa nchini.
Kwa upande
wao wanachama waliohudhulia katika kikao hicho cha naibu katika mkuu cha
kuwataka wanachama wake kugomea uchaguzi, katibu wa TALGWU wilaya ya busega
mkoani simiyu Bw, Daniel Zacharia amesema kuwa wao kama wanachama wako tayari
kwa hilo kwani wao ndiyo watendaji wakuu katika chaguzi mbalimbali hapa nchini
, Hivyo wanaiomba serikali kuweza kulipa deni lao ndipo watashiriki katika
chaguzi hizo.
Wanachama wa
TALGWU wilayani busega wakiongozwa na Mathias Kahema anasema kuwa
wanakiombasana chama chao kuwa na umoja, ushirikiano na ujasiri ili waweze
kufikia malengo yao na pia aliutaka uongozi wa TALGWU hapa nchini kuweza kuweza
kuwa karibu zaidi na wanachama ili kuweza kutatua kero za watumishi hao kwani
wanakero nyingi sana zinazowakabiri .
Pia
aliongeza kuwa maia ya kero zinazotusumbua ni kutothaminiwa na serikali yetu
hivyo sasa hiki ni kipindi chetu kuonyesha nasi tupo na tunaumuhimu kiasi gani
nchini cha msingi ni umoja na ushirikiano.
Comments
Post a Comment