GARI LAACHA NJIA NA KUINGIA DARAJANI MPAKANI MWA SIMIYU NA MWANZA.



Na Shushu joel
Busega

Gari lenye namba T 714  BJB aina ya scania lifanyalo safari zake toka msoma kwenda Mwanza limeacha njia na kuingia darajani katika kijiji cha masanza kona kata ya kiloleli wilayani busega katika mkoa wa simiyu.



Chanzo cha ajali hiyo ni kupasuka kwa taili ya mbele ya kulia na hivyo kufanya gari hilo kuingia darajani na huku ndani ya daraja hilo kulikuwa na maji mengi hivyo gari hilo kuingiliwa na maji pia.
Dereva wa gari hilo Bw, Edward  Juma anasema kuwa alijaribu kujitaidi ili kulizuia gari hilo kuingia katika mto huo lakini ilinishinda hivyo ilinibidi niiweke tu ndani yam to huo, gari ilikuwa na abilia 60 na wala hakuna mtu hata mmoja aliyepoteza maisha na hata majerui ni yale ya kawaida,
Mery Mwita ni abilia aliyekuwa anatoka msoma kwenda mwanza anaeleza kuwa anampongeza sana dereva wa gari kwa ujasili wake wa kulifanya gari hilo kutokuanguka na kuweza kuokoa maisha yetu sisi abilia wake.








Pia Franciss mongela anasema kuwa kama dereva asingekuwa makini basi leo tungesema mengine hivyo mungu ambaliki huyu kijana .
Katika gari hilo pia kulikuwemo na askali polisi Bw, Joseph Christopher mwenye namba H 812 PC kutoka kituo cha busega aliyekuwa akipeleka maabusu wilayani magu mkoani mwanza yeye anaeleza kuwa gari lilikuwa katika mwendo wa kawaida sema ajali ni ajali hivyo cha msingi ni kumpongeza dereva kwa kazi nzuri aliyoionyesha mbele ya abilia wake.

Comments