WANANCHI WAGAWANA NYAMA YA FISI BUSEGA.
Na shushu joel
Busega, simiyu








Wakazi wa kitongoji cha mwamsikula A kijiji cha Bukabile kata ya kabita wilayani Busega na katika mkoa wa Simiyu jana walitoa ya kufunga mwaka 2014.
Wakazi hao  walimkuta fisi huyo amedumbukia kwenye shimo la choo katika nyumba ya mzee Finias Udoe nyakati za usiku na hivyo wananchi hao kuweza kumtoa fisi huyo ndani ya shimo hilo majira ya saa 3 asubui  na kisha kuweza kumgawana nyama yake.
Wakizugumza kwa wakati tofauti wakazi hao wanasema juu ya matumizi ya nyama yamnyama huyo.
   
John Okuku ambaye pia ni mweyekiti wa kijiji cha Bulima anasema kuwa wananchi hao waligawana mnyama huyo kwa imani za kishirikina zilizowatawala katika nafsi zao
Mwenyekiti huyo aliwataja waliogawana nyama hiyo kuwa ni Magesa mkwaja aliyechukua sehemu za siri za mnyama huyo, Mganga mmoja wa kienyeji toka wilayani Bariadi amabaye pia ni kiongozi wa sungusungu katika wilaya hiyo aliyejulikana kwa jina laNyakali Goloneli kwa upande wake alichua kiganja cha mkona wa kushoto na kusema kuwa hii ni dawa ambayo inatibu magonjwa mengi katika mwili wa mwanadamu.

Kwa upande wake mwenye nyumba ambako fisi huyo alidumbukia Bw, Finias Mdoe anasema kuwa siku ya tukio yeye alikuwa amelala kwa watoto wake jirani na kwake ambapo asubuhi alikuta tukio la namna hiyo nyumbani kwake lakini mzee huyo alisema kuwa hata yeye anashangazwa na kitendo cha wananchi hao kugawana mnyama huyo

Pia mzee huyo alikwenda mbali zaidi baada ya kusema kuwa fisi huyu alikuwa amekatwa masikio kama vile tunavyokata wanyama wetu wa kufuga kama mbuzi na kondoo nah ii ikiwa na maana kuwa ni alama yako wewe mfugaji sasa kwa fisi huyu sijui labda ni alama ya mwenyewe.
Mpaka wananchi hao wanamaliza kugawana mnyama huyo hakuna mtu yeyote Yule kutoka mamlaka ya wanyama poli aliyefika katika tukio hilo la kusikitisha la kugawana kwa nyama ya fisi.
 

Comments